UTALII WETU
UFAHAMU MLIMA KILIMANJARO
Kilimanjaro
ni mlima mrefu kuliko yote Afrika, pia ni wa pili kwa urefu Duniani.
Mlima huu uko nchini Tanzania katika Mkoa wa Kilimanjaro. Una urefu wa
futi 19,340 (mita 5,895). Hali halisi Kilimanjaro ni zaidi kuliko
mlima tu ni kama safu ndogo ya milima mitatu: Kibo, Mawenzi na Shira.
Hii mitatu inaonekana kama vilele vitatu vya mlima mmoja hivyo si
vibaya kusema Kilimanjaro ni mlima. Kilimanjaro ni volkeno iliyolala
kwa sasa. Kwenye kilele cha Kibo gesi bado inatoka. Kumbukumbu ya
wenyeji ina habari ya mlipuko takriban mnamo mwaka 1730. Kilele cha
juu cha Kibo kinaitwa Uhuru. Mtu wa kwanza wa kufika kileleni hapo
alikuwa Johannes Kinyala Lauwo kutoka Marangu aliyewaongoza Wajerumani
Hans Meyer na Ludwig Purtscheller tarehe 6 Oktoba, 1889 wakati wa
ukoloni wa Ujerumani. Wakati ule waliita ncha ya juu
"Kaiser-Wilhelm-Spitze" (kijer.:Kilele cha Kaisari Wilhelm) kwa
heshima ya Kaisari wa Ujerumani. Kibo ina theluji na barafuto kadhaa
ndogo.
BY JOSHUA KUNGU
0 comments:
Post a Comment